Mamlaka ya maendeleo ya
biashara Tanzania TANTRADE imeingia ubia na kampuni ya simu za mkononi ya
Vodacom katika kuhakikisha jamii inapata taarifa za maonyesho ya biashara ya
kimataifa ya sabasaba yanayotarajiwa kuanza taerehe 28 katika viwanja vya
mwalimu nyerere jijini Dar es salaam.
Mkuu wa kitengo cha mawasiliano wa Vodacom, Joselyne Jonathan
Kamuhanda amesema zaidi ya
shilingi milioni hamsini zitatumika kudhamini mawasiliano katika maonyesho hayo
kupitia vipindi katika vyombo vya habari na matangazo.
No comments:
Post a Comment