Sunday, July 22, 2012

BENKI YA AZANIA YAZINDUA HUDUMA MPYA YA KUTUMIA INTANET

Charles Singili Mkurugenzi Mtendaji Azania Bank
Benki ya Azania ya hapa nchini imezindua huduma mpya za kibenki kwa kutumia internet (Internet Banking) kwa lengo la kuwawezesha wateja wake kupata huduma za fedha kwa uraisi.

Kuzinduliwa kwa huduma hizo kutasaidia upatikanaji wa taarifa muhimu za akaunti za wateja wa benki hiyo na hivyo kuwawezesha kupata huduma kwa haraka.

Kwenye makao makuu wa Benki ya Azania Jijini Dar es salaam, mkurugenzi mtendaji wa benki hiyo alizindua huduma hii mpya na hivyo kutoa fursa kwa wateja wa benki hiyo kupata taarifa za akaunti zao popote walipo.

Kwa upande wake mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya mawasiliano Tanzania profesa John Nkoma amewataka wateja wanaotumia huduma za mitandao ya internet kuwa makini na kutunza namba zao za siri ili kuepusha wizi wa kutumia mtandao.

Huduma hiyo itamuweza mteja mwenye akaunti kulipia huduma mbalimbali kama Luku, kulipia huduma ya Maji kwa Dar es salaam – DAWASCO, DSTV na hata kununua muda wa maongezi kwenye siku yake bila kwenda kwenye tawi la Benki.

Benki hiyo ambayo pia inamilikiwa serikali inaendelea na maboresho ya huduma zake ili kuwawezesha wateja wake kutumia huduma hizo bila usumbufu wowote.

No comments:

Post a Comment