Saturday, July 21, 2012

BILIONI 250 KUIMARISHA MIUNDOMBINU YA BARABARA, MAJI SAFI NA DEMOKRASIA ZANZIBAR





Umoja wa Ulaya na serikali ya Tanzania zimetiliana saini ya makubalino ya msaada wa shilingi bilioni 250 kwa lengo la kuimarisha miundombinu ya barabara, maji safi  pamoja na kuimarisha demokrasia ili kuinua uchumi wa Tanzania.

Katika makubaliano hayo yaliyofanyika ikulu jijini dar es salaam jumla ya mikataba sita ilisainiwa na waziri wa fedha William Mgimwa pamoja na kamishna wa maendeleo ya Umoja wa Ulaya kwa niaba ya marais wa Tanzania pamoja na umoja huo.

Mkataba wa kwanza ambao ni euro million45 unakwanda katika sekta ya usafirishaji, euro million22  katika kuimarisha barabara za vijijini na euro milioni 3 zinakwenda katika kuimarisha demokrasia  visiwani Zanzibar

Nyingine ni euro milioni 2.5 zimetengwa katika kuimarisha ushirikiano na sera za umoja huo nchini  Tanzania pamoja na euro milioni 51.51 ambazo zitatumika kwa lengo la kutimiza malengo ya milenia mdg kwa kupata maji safi katika mikoa ya lindi, rukwa na kigoma.

Akiongea mara baada ya kusaini kwa mikataba hiyo rais wa kamisheni ya Ulaya Jose Manuel Barroso amesema kuwa mikataba hiyo ipo wazi na inalenga kusaidia maeneo ambayo yameonekana kukwamisha maendeleo kwa kiasi kikubwa.

Naye rais Jakaya Kikwete amesema kuwa miradi hiyo inalenga kumaliza matatizo ya maji hasa katika mikoa iliyotajwa ambapo bado wananchii wake wameonekana kukwazwa na matatizo hayo.

Tangu kujiunga na kamisheni ya umoja wa ulaya mwaka 1975 tanzania imeweza kupata msaada wa euro billion1.8 sawa na shilingi trillion 3.8 ambazo zimepelekwa katika mahitaji mbalimbali.

No comments:

Post a Comment