Thursday, June 21, 2012

Madaktari kugoma tena


JUMUIYA ya Madaktari Tanzania imetangaza kuanza rasmi mgomo usio na kikomo kwa nchi nzima June 23, mwaka huu mpaka serikali itakapotoa ufumbuzi wa kutatua madai yao yaliyowasilishwa serikalini Januari 27, mwaka huu.
Awali madaktari hao walitoa muda wa wiki mbili kwa serikali kuhakikisha inatimiza madai yao ambapo hadi sasa wamesema hakuna ufumbuzi wa madai yoyote yaliyofanyiwa kazi licha ya kukaa meza moja na serikali na kukubaliana kutatuliwa kero zao.

No comments:

Post a Comment