Wednesday, July 18, 2012

TANZANIA YAASWA KUWEKA MKAZO KATIKA VITA YA MALERIA

Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania

Rais Ellen Johnson Sirleaf wa Liberia

Dr. Hussein Mwinnyi Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii

Rais Kikwete na Rais Sirleaf wakikata utepe kuashiria uzinduzi wa ofisi za ALMA Dar es Salaam
Rais wa Liberia na mwenyekiti  wa umoja wa ushirikiano wa viongozi wa afrika unaoshugulikia Ugonjwa wa malaria ALMA Ellen Johnson Sirleaf amesema kuwa serikali ya Tanzania inapaswa kuweka mkazo katika vita dhidi ya malaria ili kuondokana na maambukizi ya ugonjwa wa malaria.

Rais Sirleaf ameyasema hayo jijini dar es salaam wakati akifanya uzinduzi wa ofisi ya ALMA ambayo itashughulikia kwa kiasi kikubwa kuweka mikakati ya kutokomeza ugonjwa wa malaria.

Mpaka kufikia sasa vyandarua million 400 vimegaiwa kwa nchi zilizopo kusini mwa jangwa la sahara ambapo Tanzania ilipata vyandarua million 17 kwa wanawake wajawazito pamoja na vyandarua million 9 kwa watoto wenye umri chini ya miaka 5 vilivyotolewa bure kwa lengo la kupunguza maambukizi.

Naye Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete amesema kuwa Tanzania imefanikiwa kupunguza vifo vinavyotokana na ugonjwa wa malaria kwa kipindi cha miaka3 na Zanzibar wamefanikia kuondoa ingawa wanahitaji kujiridhisha kwa kuongeza nguvu Tanzania bara ili kuondokana na  maambukizi yatakayosambaa.

Naye waziri wa afya na ustawi wa jamii Dr.hussen Mwinyi amesema kuwa dawa ya mseto dozi ya malaria kwa mtu mzima inatakiwa kuuzwa kwa shilingi 1600 kutokana na kuwa na ufadhili wa global fund ambao unapelekea kuuzwa kwa dawa hiyo kwa bei ya chini.

Nchi za Afrika ndizo zinaongoza kuwa na magonjwa wa malaria kwa asilimia 83 ambapo vifo vinavyotokana na maradhi ya malaria ni asilimia 89 ambayo kwa kiasi kikubwa vinatokana na wananchi wanaoshindwa kununua vyandarua pamoja na dawa.

Umoja wa ushirikiano wa viongozi wa afrika unaoshughulikia utokomezaji wa ugonjwa wa malaria ALMA ulianzishwa mwaka 2009 newyork marekani ambapo Rais kikwete alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa kwanza.

No comments:

Post a Comment