Wednesday, July 18, 2012

BAJETI NDOGO KATIKA MASUALA YA MAENDELEO YACHANGIA MFUMUKO WA BEI NA KUPANDA BEI ZA VYAKULA

Imeelezwa kuwa mfumuko wa bei za bidhaa na kupanda kwa bei za vyakula hapa nchini ni matokeo ya matumizi makubwa ya serikali yasiyo na tija kwa wananchi na kusababisha kutengwa kwa bajeti ndogo katika masuala ya  maendeleo.

Hayo yamebainishwa jijijni Dar es salaam na Mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF ambaye pia ni mtaalam wa uchumi ambapo amesema  matumizi ya serikali yameongezeka kutoka trioni 13.1 mpaka trilioni 15.1.

Kwa upande wa baadhi ya wafanyabiashara wa nafaka katika soko la Buguruni jijini Dar es salaam wamesema kupanda kwa bei za mafuta na umeme ni sababu kubwa inayochangia kutoshuka kwa bei za vyakula hata katika kipindi hiki cha msimu wa mazao.
Amesema ili kupunguza gharama za maisha ni lazima uzalishaji uongezeke lakini sekta ya kilimo haijatengewa fedha za kutosha kwa madhumuni ya kuongeza tija ya uzalishaji wa chakula na mazao mengine ya kilimo
Amesema kwa mujibu wa taarifa ya uchumi wa taifa inaonyesha kuwa kwa muda wa zaidi ya miaka 20 iliyopota sekta ya kilimo, misitu na uvuvi zimekuwa zikitengewa chini ya asilimia 5 ya matumizi yote ya serikali.

Kwa mujibu wa makubaliano ya nchi za SADC ni kutenga angalau asilimia 10 ya matumizi ya serikali katika sekta ya kilimo ili kuongeza kasi ya ukuaji wa sekta hiyo kwa kuongeza uzalishaji wa chakula na kupunguza umaskini uliokithiri

No comments:

Post a Comment