Wednesday, July 18, 2012

NOKIA NA VODA WASHIRIKIANA KUTOA HUDUMA ZA QURAN KWENYE SIMU

Samson Majwala-Meneja wa Nokia


Katika kipindi hiki cha KUELEKEA Mwezi mtukufu wa  Ramadhani Kampuni ya simu za mikononi ya Vodacom Tanzania imeingia ubia na kampuni ya Nokia na kurahisisha upatikanaji wa Quran kwenye simu ya mikononi.

Meneja wa Nokia hapa nchini Samson Majwala ameelezea uzinduzi wa huduma huo kuwa utajumuisha   ofa ya simu za Nokia Asha 200 na Nokia Asha 302.

Ushirikiano huo baina ya Vodacom na Nokia pia umewalenga vijana wengi pamoja na  wafanyakazi wote wenye matumizi makubwa ya mitandao ya kijamii Facebook. Twitter pamoja na Wikipedia ofa ambayo itadumu miezi sita.
Mkuu wa kitengo cha Masoko na Bidhaa kutoka Vodacom Mgopelinyi Kiwanga amewaambia  wateja wao kuwa huo ni mfululizo wa kuileta jamii karibu zaidi katika mawasiliano hususani ya mtandao wa internet.

Ushirikiano baina ya Nokia na Vodacom huenda ukafanikisha kumaliza kero za mawasiliano hapa nchini.

No comments:

Post a Comment