Sunday, July 1, 2012

TANESCO yaongeza 100MW kwenye gridi ya taifa







Shirika la umeme Tanzania TANESCO linatarajia kuongeza megawatt 100 kwenye grid ya taifa baada ya kukamilika kwa mtambo wa kuzalisha umme kwa kutumia mafuta.
Kukamilika kwa mtambo huo uliojengwa kwa fedha za serikali kutaongeza megawatt za umme kwenye grid mpaka kufikia 800 na hatimaye kupunguza tatizo la mgao wa umeme.
Badra Masoud ambaye ni meneja uhusiano wa TANESCO amesema tayari wamelipa deni la Songas na kuongeza pia kuwa moja ya vipaumbele vilivyowekwa katika bajeti ya mwaka 2012/2013 ni uimarishaji wa miundombinu ya nishati ya umeme ili kuweza kuzalisha zaidi pamoja na kupunguza kupanda kwa gharama ya maisha kwa wananchi.

No comments:

Post a Comment