Dr. Mary Nagu |
Pinda na Nagu wakiangalia bidhaa mbalimbali |
Bidhaa za nguo |
Waziri Mkuu Mizengo Pinda |
Waziri
mkuu Mizengo pinda amewataka wajasiriamali nchini kuwa na mikakati ya kupanua
wigo wa biasahara zao nchini na nje ya
nchi kwa kufuata utaratibu wa kubandika stempu za barcodes katika bidhaa zao.
Akisisitiza
ubora wa bidhaaa za viwanda vidogovidogo nchini Waziri Mkuu amewataka
wajasiriamali hao kuzingatia upitishaji wa bidhaa zao katika shirika la viwango
TBS ili kuhakikisha viwango vya bidhaa zao.
Pinda ameyasema hayo wakati wa sherehe za utoaji ruzuku kwa wajasiriamali 870 waliopatiwa msaada huo chini ya mpango wa
kuinua wajasiriamali wa BDG. Pia amesema serikali imeazimia katika bajeti ya mwaka huu wa fedha kuondoa kodi ya ongezeko la thamani (VAT) katika bidhaa zinazozalishwa na viwanda vya ndani ikiwa ni jitihada za kukuza viwanda vya nguo nchini.
Nae waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu uwekezaji
na uwezeshaji Dr. Mary Nagu amesema kuwa ili kuvutia uwekezaji kwa wazalendo na
wageni serikali ni lazima iangalie sera na sheria katika kumtengenezea mwekezaji
mazingira mazuri
Zaidi
ya shilingi bilioni 5 zimegawiwa kwa wajasiriamali kote nchini kupitia mradi wa
ushindani wa faidika kibiashara BDG unaofadhiliwa na serikali ya Uingereza na
kuratibiwa na taasisi ya sekta binafsi nchini – TPSF.
No comments:
Post a Comment