Mhandisi William Mhando |
Taarifa hiyo pia imesema kuwa tuhuma hizo dhidi ya mhandisi Mhando ni nzito hivyo ni vyema zifanyiwe uchunguzi huru na wa kina kama inavyoeleza, "Hivyo, bodi iliazimia pamoja na mambo mengine kama ifuatavyo: Uchunguzi wa tuhuma hizo uanze mara moja kwa kutumia uchunguzi huru na kumsimamisha kazi Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Mhandisi William Mhando ili kupisha uchunguzi huo na kwa kuzingatia matakwa ya sheria za kazi nchini".
Pamoja na mhandisi huyo, viongozi wengine wamesimamishwa kazi ili kupisha uchunguzi huo wakiwemo Robert Shemhilu ambaye ni Naibu Mkurugenzi Mtendaji Huduma za Shirika, Ofisa Mkuu wa Fedha Lusekelo Kassanga na Meneja Mwandamizi Manunuzi Harun Mattambo.
No comments:
Post a Comment