Saturday, July 14, 2012

LITA 180 ZA GONGO ZAKAMATWA KIGOGO

Pereira Ame Silima Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani

ACP Charles Kenyela

Mkazi wa Kigogo akiwatangazia watu waache kunywa gongo

Kamanda Kenyela akimtuza sh. 5000 mkazi huyo baada ya kutoa matangazo


Naibu waziri wa mambo ya ndani Mh. Pereira Ame Silima amesema serikali inaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha vifo zaidi ya kumi vya wakazi wa Kigogo Mbuyuni Jijini Dar es salaam wanaosadikiwa kunywa pombe haramu ya Gongo inayosadikiwa kuchanganywa na Spiriti na dawa ya Jiki.

Hata hivyo chanzo kamili cha vifo hivyo kinatarajiwa kujulikana baada ya majibu ya mkemia mkuu wa serikali anayechunguza pombe hiyo.

Akizungumza na wakazi wa eneo hilo la kigogo Mbuyuni Naibu waziri Silima amewataka watanzania kuachana na tabia ya kuchanganya vitu bila utaalamu ili kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza.

Kwa upande wake kamanda wa polisi mkoa wa kinondoni Kamishna msaidizi wa Polisi Charles Kenyela tangu kutokea kwa tukio hilo wamefanya oparesheni na kufanikiwa kukamata lita 180 za Gongo na watuhumiwa 12 katika eneo hilo la Kigogo.

Mwanzo mwa wiki hii watu zaidi ya kumi wamefariki dunia kwenye eneo la kigogo mbuyuni baada ya kunywa pombe haramu ya gongo ambayo inadhaniwa kuchanganywa na sumu na wengine 7 bado wamelazwa kwenye hospitali ya Rufaa ya Amana.

No comments:

Post a Comment