Saturday, July 14, 2012

LIPUMBA AITAKA SERIKALI KUUNDA TUME HURU YA UCHAGUZI NA KUACHANA NA TUME YA KURATIBU UKUSANYAJI WA MAONI YA KATIBA MPYA

Prof. Ibrahim Lipumba Mwenyekiti CUF

Mwenyekiyi wa chama cha wananchi CUF Prof. Ibrahim Lipumba amesema kuwa serikali inahitaji kuunda tume huru ya uchaguzi na kuachana na kutegemea tume ya kuratibu ukusanyaji wa maoni ya uundwaji wa katiba ambayo itachelewa kumaliza kazi zake kulingana na hadidu za rejea walizopewa.

Prof Lipumba ameyasema hayo katika kikao cha baraza kuu la chama hicho ambacho kinafanyika kwa siku mbili jijini dar es salaam.

Prof. Lipumba anasema kuwa muda wa kutafuta katiba mpya ni mfupi na hivyo ni afadhali serikali ikaelekeza nguvu zake katika uundaji wa tume huru ya uchaguzi ambayo itakuwa na uwezo wa kusimamia taratibu na kutoa takwimu sahihi za wapiga kura kote nchini.

Hata hivyo Prof Lipumba ameongeza kuwa swala la uongezaji wa fedha za bajeti kutoka shilingi Trilion 13 mwaka 2011/2012 na kufikia shilingi trillion 15 kwa mwaka 2012/2013 ni kazi bure kwani fedha za maendeleo bado ni kidogo kulinganisha na mahitaji ya watanzania.

Ameongeza kuwa mfumuko wa bei pamoja na kupanda kwa gharama za maisha kunatokana na matumizi makubwa ya serikali na pia serikali kushindwa kutenga asilimia 10%ya bajeti katika kilimo kama ambavyo nchi za SADC zimekubaliana.

Katika kipindi cha siku mbili baraza hilo litapata nafasi ya kujadili agenda 10 likiwemo swala la migomo ya madaktari ambao inaonekana kuathiri kwa kiasi kikubwa upatikanaji wa huduma za afya kwa watanzania na hasa wa kipato cha chini.

No comments:

Post a Comment