Thursday, July 19, 2012

MIGOGORO YA MIPAKA KATIKA MISITU YA PUGU NA KAZIMZUMBWI


SERIKALI imekiri kuwepo kwa mapungufu katika Wizara mbili ikiwepo Wizara ya ardhi na maendeleo ya makazi pamoja na Wizara ya maliasili na utalii hali inayosababisha utata na migogoro miongoni mwa jamii inayozunguka misitu ya Pugu na Kazimzumbwi Wilayani Kisarawe Mkoani Pwani.
Sehemu ya Msitu wa Pugu
 
Migogoro ya mipaka inaendelea kwa wakazi wanaoizunguka misitu hiyo na kusababisha kuvunjika kwa amani kutokana na baadhi ya wakazi kuvamia msitu wa kazimzumbwi na kuchoma moto maeneo ya msitu huo kwa madai kuwa Wizara ya maliasili na utalii inawaondoa katika maeneo yao huku wakijua kuwa maeneo hayo ni ya kwao.
Kauli ya Serikali imetolewa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu wakati akikagua maeneo ya msitu wa kazimzumbwi yaliyoathiriwa na watu wanaodaiwa kuvamia msitu huo na kuchoma moto kwa madai kuwa maeneo hayo ni ya kwao.


Nyalandu amesema kuwa ingawa Wizara hizo zitakaa pamoja ili kurekebisha kasori hizo lakini ramani ya awali ambayo inatambulika na Wizara ya Maliasili na sio ile iliyochorwa na Wizara ya ardhi.


Kwa upande wake Meneja Misitu ya Pugu,Kaimzumbwi na Vikindu Bw.Matthew Mwanuo amesema mipaka iliyotengwa na Wizara ya ardhi na maendeleo ya makazi ina utata kufuatia kutoa zaidi ya mita 900 takribani kilomita moja za msitu kuingia katika makazi ya wananchi wa kijiji cha maguruwe kilichopo Wilaya ya Kisarawe. 


Nae Mtendaji Mkuu wa Wakala wa huduma za Misitu TFS Bw.Juma Mgoo amesema ni muhimu Wizara hizo mbili zikasimamia sheria za mipaka na sio kupindisha sheria hatua inayoweza kusababisha umwagaji wa damu kutokana na kugombania mipaka.

Hivi karibuni kundi la watu wanaodaiwa kuondolewa katika maeneo yanayozunguka msitu wa kazimzumbwi walivamia msitu huo kwa madai kuwa waliondolewa katika maeneo hayo kwa njia isiyo halali.

No comments:

Post a Comment