Thursday, July 19, 2012

KESI YA IDDI SIMBA KUSIKILIZWA AGOSTI 16

Mahakama ya hakimu mkazi kisutu imesogeza mbele kesi inayomkabili aliyekuwa mwenyekiti wa Bodi ya shirika la usafiri Dar es salaam UDA Iddi Simba anayekabiliwa na shitaka la matumizi mabaya ya madaraka na kulisababishia shirika hilo hasara ya shilingi Bilion 2.4
Iddi Simba

Mbali na Simba ambaye aliwahi kuwa waziri wa viwanda na biashara  washtakiwa wengine ni aliyekuwa meneja mkuu wa UDA Victor Milanzi na mkurugenzi wake Salim mwaking’inda.

Majira ya saa tatu asubuhi ambapo Idi Simba pamoja na wenzake wamefika katika mahakama ya mkazi kisutu kwa ajili ya kuanza kusikiliza kesi hiyo ambapo hakimu mfawidhi Ilvin Mgeta ametaja tarehe 16 ya mwezi august kwa ajili ya kuanza kusikiliza kesi hiyo.

Simba pamoja na aliyekuwa meneja wa mkuu wa wa Uda Victor Milanzi wanakabiliwa na kosa la kughushi barua wakionesha kuwapo kwa kiwango cha fedha kwenye akaunt zote za benki za Uda fedha ambazo hazikuwepo wakitenda kosa hilo septemba 2 mwaka 2009.

Siku hiyo hiyo wakakutwa na kosa la kuchepusha fedha shilingi million 320 wakijifanya ni malipo ya awali ya mauzo ya Hisa katika shirika hilo fedha ambazo walijipatia kutokana na nyazifa walizokuwa nazo.

Washitakiwa Simba na Mwaking'inda kati ya septemba 2009 na FebruarI 2011waliharibu hisa za Milioni 7.8 zisizotumika na shirika hilo zinazokadiriwa kuwa na thamani ya shilingi Trilion 1.14 bila kufuata taratibu za zabuni kitendo ambacho ni uvunjaji wa masharti ya kanuni ya 63(1)ya ununuzi ya uma.

Kwa ujumla washtakiwa wote wanadaiwa kuwa February 11 2011 walishindwa kuchukua tahadhali zinazostahili kwa kumuuzia kampuni ya simon Group hisa milioni 7.8 zisizotumika kwa bei ya shilingi trilio 1.14 ambapo wangeweza kutoa ofa kwa mnunuzi kununua kwa bei ya juu zaidi na hivyo kusababisha hasara ya shilingi trillion 2.3 kwa shirika hilo.

Washitakiwa hao walitakiwa kutoa hati ya nyumba na kuwa na wadhamini wawili wanaoaminika na kila mmoja asaini bondi ya shilingi million 500 ambapo Idi Simba aliwasilisha hati ya nyumba yenye thamani ya shilingi billion8 na kuridhia wenzake waweze kuitumia kupata dhamana.

Kesi hiyo itaanza kusikilizwa august 16 mwaka huu ambapo washtakiwa wote wapo nje kwa dhamana.

No comments:

Post a Comment