Thursday, July 5, 2012

LIPUMBA AWAASA WATANZANIA KUACHA KUTUMIA SAMANI ZA NJE

Prof. Ibrahim Lipumba




Prof. Lipumba akipata maelekezo katika banda la NEEC sabasaba

Prof. Lipumba akipata maelekezo katika banda la NEEC sabasaba

Dr. Joyce Chonjo, Mkurugenzi NEEC



Serikali na taasisi binafsi zimemetakiwa kuacha kuagiza samani za maofisini nje ya nchi na badala yake wanunue samani za kitanzania zinazotengenezwa hapa nchini ili kukuza soko la ndani na kuongeza ajira kwa vijana

Hayo yamebainishwa na mwenyekiti wa chama cha wanachi CUF Profesa Ibrahim Lipumba ambaye pia ni mtaalam wa maswala ya uchumi wakati akitembelea maonyesho ya kimataifa ya biashara jijini Dar es salaam

Profesa Lipumba amesema ni wakati muafaka wa kuacha kung’ang’ana na bidhaa za nje ya nchi kwa kuwaunga mkono vijana  kwa kutumia bidhaa za ndani ambazo zinaubora wa hali ya juu. pia amesema maonyesho kama haya yana umuhimu mkubwa katika kutangaza bidhaa za ndani na kukuza uchumi wa nchi unaoenda sambamba na kukua kwa uchumi wa mtu mmoja mmoja


Nae Dr. Joyce Chonjo ambaye ni mkurugenzi wa baraza la taifa la uwezeshaji amesema zaidi ya wajasiriamali 38 katika maonyesho hayo wamenufaika na mfuko wa uwezeshaji ambapo zaidi ya mikoa 5 inatarajiwa kunufaika na bajeti ya mwaka huu.


Amesema pesa hizo pia zitatumika katika kutoa mokopo, mafunzo, katika kufanya utafiti na uhamasishaji kwa kuwa kila siku uwezeshaji wa vikundi na mtu mmoja mmoja unasomga mbele 

No comments:

Post a Comment