Kamanda Kova akionesha silaa zilizokamatwa |
Kamanda Kova akionesha pesa bandia zilizokamatwa |
Kamanda Kova akionesha pesa bandia zilizokamatwa |
Jeshi la polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam limewakamata watuhumiwa zaidi ya 51 kwa makosa mbalimbali likiwemo la wizi wa fedha katika mashine ya ATM za benki mbalimbali nchini.
Miongoni
mwa watuhumiwa hao ni pamoja na Raia wa kigeni aliyejulikana kwa jina la Goce
au Pendarowsk aliyehusika na wizi wa zaidi ya shilingi milioni 100.
Aidha
jeshi lapolisi limefanikiwa kukamata Dola za kimarekani bandia zenye thamani ya
shilingi za kitanzania milioni 35 pamoja fedha bandia za kitanzania zaidi ya
milioni 1 zikiwemo nyenzo zilizotumika kutengeneza fedha hizo.
Pia
katika operation nyingine jeshi la pilisi limefanikiwa kukamata magari 18
yaliyoibiwa jijini Dar es salaam mengine
yalikamatwa nje ya mikoa ya Dar es salaam likiwemo la aliyekuwa katibu Mkuu wa
shirikisho la soka nchini TFF Fredrick Mwakalebela, na hapa analishukuru jeshi
hilo kwa jitihada lililoonyesha.
No comments:
Post a Comment