Godfrey Simbeye, Mkurungenzi TPSF |
Mfuko wa Taasisi ya sekta binafsi Tanzania ‘TPSF’ imetoa shilingi bilioni tano na nusu kwa wajasiliamali waliopata alama za juu katika mafunzo ya kuwajengea uwezo kwa lengo la kujiendeleza katika kujikwamua na umaskini.
Jumla
ya wajasiliamali 1565 kutoka katika mikoa ya Tanzania bara na visiwani wamepata
mafunzo hayo huku kati yao wanawake wakiwa ni 56% na vijana walio na umri chini ya miaka 35
wakiwa ni 43%.
Mkurugenzi mtendaji wa TPSF Godfrey
Simbeye amesema tayari faida imeanza kuonekana kutokana na wajasiliamali hao
kuanza kujitegemea.
No comments:
Post a Comment