SERIKALI
imeanza jitihada kubwa za kuwalinda wakulima wa zao la pamba nchini
kufutilia kuporoka kwa bei ya zao hilo kwenye masoko ya kimataifa.
Ili
kuhakikisha kuwa wakulima hao hawaumii kupita kiasi katika hali ya sasa
ya mporomoko wa bei ambao ni dhahiri utaathiri bei za zao hilo kwa
wakulima nchini, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa
Jakaya Mrisho Kikwete amefanya mfululizo wa mikutano kujadili suala
hilo.
Akiwa
mjini Dodoma kikazi, Rais Kikwete usiku wa kuamkia leo, Ijumaa, Juni
22, 2012, alifanya mikutano miwili ambako kwanza alikutana na kuzungumza
na wanunuzi wa zao la pamba na katika mkutano wa pili akakutana na
kuzungumza na wabunge wa maeneo yanayolima pamba nchini wakiongozwa na
Mbunge wa Bariadi Magharibi, Ndugu John Cheyo.
Mikutano
hiyo miwili imefuatiwa na mkutano wa viongozi wa wakuu wa Serikali
uliofanyika asubuhi la leo kwa nia ya kuona ni hatua zipi zinaweza
kuchukuliwa angalau kuinua bei la zao hilo kwa wakulima.
Katika
msimu uliotarajiwa kuanza mwanzoni mwa wiki hii, wanunuzi wa pamba
walikuwa wamesema kuwa watanunua kilo moja ya pamba kwa kiasi cha sh.
525 kulinganisha na bei ya mwaka jana ya sh. 1,200 kwa kilo moja.
Bie
hiyo imepingwa kwa kiasi fulani na wabunge kutoka maeneo yanayolima
pamba ambao wamekuwa wanawataka wakulima wa zao hilo wasikubali kuuza
pamba yao chini ya sh. 1,000 kwa kilo moja.
Jitihada
za Serikali zinalenga kuona jinsi gani kiasi hicho cha sh. 525 kinaweza
kupanda angalau kufikia sh. 725 na hivyo kukaribia kabisa bei ya sh.
800, ambayo wakulima walilipwa mwanzoni mwa msimu wa mwaka jana, kabla
ya kiwango hicho kupanda na kufikia 1,200 kwa kadri bei ya pamba duniani
ilivyozidi kupanda.
Serikali
inaona kuwa siyo vyema wala siyo haki kwa mkulima wa pamba kubebeshwa
mzigo wote wa kuporomoka kwa bei ya zao hilo duniani badala ya mzigo huo
kugawanywa mionogni mwa wadau wengine wa zao hilo.
No comments:
Post a Comment