Serikali
inakabiliwa na uhaba wa wahudumu wa fani ya maabara hali inayochangia
kuzorota huduma hiyo katika baadhi ya vituo vya afya nchini.
Hali
hiyo imebainishwa na Bw.Dickson Majige ambaye ni Mkuu wa huduma za maabara
nchini wakati wa maadhimisho ya huduma za maabara.
Nao
baadhi ya wanafunzi wa chuo cha Uuguzi na Tiba katika Hospitali hiyo walioshiriki maadhimisho hayo wakaitaka
serikali kuboresha mazingira ya kazi na kuwaongezea vitendea kazi.
Maadhimisho
hayo yemefanyika ili kuangalia changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya
afya kwa upande wa maabara na kuifikishia serikali ili izifanyie kazi.
No comments:
Post a Comment