Sara Ibrahim, Mama wa mtoto |
Twaha Mussa, Baba wa mtoto |
Wodi ya wazazi, Mwananyamala |
Mwili wa mtoto mchanga aliyezaliwa jana katika
Hospitali ya Mwananyamala ya jijini Dar es Salaam umepotea katika mazingira ya
kutatanisha na kifanya hospitali hiyo kuingia katika kashfa nyingine.
Ndugu wa mzazi wa kichanga hicho Bi Sara Ibrahim amesema ndugu yao alifika hospitalini hapo tarehe 21 saa tatu asubuhi na kujifungua nusu saa baadae ambapo mtoto huyo ajulikani alipo mpaka sasa.
Ndugu mwingine aliejitambulisha kwa jina la Salmin amesema alifika hospitalini hapo
majira ya asubuhi kuomba mwili wa kichanga kilichozaliwa na hupata majibu
yasiyoridhisha kutoka katika uongozi huo.
Kamanda
wa polisi wa mkoa wa kipolisi kinondoni ACP Charles Kenyela amethibitisha
kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema uchunguzi juu ya tulio hilo unaenelea
No comments:
Post a Comment