Msafiri Mtemelwa, Mkurugenzi wa kampeni na uchaguzi CHADEMA |
Msafiri Mtemelwa, Mkurugenzi wa kampeni na uchaguzi CHADEMA amewataka viongozi wa serikali, watendaji
wa vijiji na vitongoji kuwakubali na kutovuruga utaratibu wa mabalozi wa
chadema waliowekwa kwa mujibu wa sheria alipokuwa akiongea na waandishi wa habari jana kaitka ofisi za chama hicho za Kinondoni.
Amesema
mabalozi wa chadema wamekuwa wakinyanyaswa na baadhi ya viongozi na kuwataka
kutofanya hivyo, na kudai kuwa tangu ulipoanza mfumo wa vyama vingi waliiomba
serikali kuwaingiza mabalozi katika mfumo wa serikali lakini hawakufanya hivyo.
Msafiri amesema pia chama cha CCM kimekuwa kikitengeneza mfumo wa kulindana katika uongozi na
ndio sababu ya chama hicho kuwang’ang’ania mabalozi wa nyumba kumi kumi kwa kuwa hawakuwa na uhakika wa
kutengeneza msingi wao mapema.
CHADEMA
inaendelea na uchaguzi wa mabalozi
ulioanza tangu juni mosi mwaka huu na unaendelea mpaka ngazi za juu kwa
kuchagua viongozi mbalimbali ndani ya chama.
No comments:
Post a Comment