Monday, June 25, 2012

Ushirikina watawala uchimbaji madini Kishapu


Machimbo ya Maganza

Noeli Ganja, Mchimbaji mdogo

Noeli Ganja akisafisha udongo


Wachimbaji wadogo katika machimbo ya Almasi yaliyopo  mji wa Maganzo Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga, wamesema wanakabiliwa na wimbi la ushirikina katika utafutaji wa Almasi hatua inayodidimiza maendeleo ya wachimbaji Wilayani humo.

Tatizo hilo linakuja kufuatia kukosekana kwa vifaa muhimu vya utafiti wa Almasi na kusababisha kuchimba kila mahali bila kuwa na uhakika wa Almasi.

Licha ya uchawi kutawala shughuli hizo wachimbaji hawa pia wanakabiliwa na uvamizi wa wawekezaji wanaonunua ardhi kutoka Serikali kuu na wanapoingia katika maeneo yao hutimuliwa bila kulipwa fidia.

Naye mbunge wa Kishapu Selemeni Masoud Nchambi anaitaka Wizara ya Nishati na Madini kutenga asilimia 2 ya mapato yatokanayo na Almasi na kuelekezwa katika maeneo ya uchimbaji ili kutoa motisha kwa wakazi waishio machimboni.

Kumekuwa na malalamiko kwa baadhi ya wachimbaji katika maeneo mengi ya uchimbaji hapa nchini, utafiti uliofanywa na Mtandao wa Jinsia Tanzania TGNP  umebaini mengi yanayohusu ukosefu wa elimu ya uchimbaji pamoja na migogoro ya ardhi.
 

No comments:

Post a Comment