Wednesday, June 27, 2012

Hali ya Ulimboka bado tete

Dr. Steven Ulimboka


Kiongozi wa jumuiya ya madaktari Tanzania Dr.Stiven ulimboka amekutwa amejuruhiwa vibaya kutokana na kupigwa na watu wasiojulikana na baadaye kutelekezwa maeneo ya mabwepande nje kidogo ya jiji la dar es salaam usiku wa kuamkia leo.

Mara baada ya Dr Steven Ulimboka kufikishwa katika chumba cha dharula katika taasisi ya  mifupa kwenye hospitali ya taifa ya muhimbili – MOI madaktari wakawazuia waandishi wa habari kufanya kazi yao.

Sintofahamu hii imekuja baada ya tukio la kushambuliwa kwa Dr Ulimboka ambaye kwa sasa ni kiongozi wa jumuiya ya madaktari inayoendesha mgomo wa madaktari hapa nchini.

Kufuatia tukio hilo madaktari na wauguzi walisitisha kutoa huduma kwa wagonjwa tangu Dr Ulimboka alipofikishwa hospitalini hapo na kuahidi kuendelea kumlinda usiku kucha.

Kamanda wa polisi kanda maalumu ya Dar es salaam Naibu kamishna wa polisi Bw Suleiman Kova amesema, Jeshi lake linaendelea na uchunguzi wa tukio hilo

No comments:

Post a Comment