Jumla ya miradi 28 ya sekta imefunguliwa katika mbio za
Mwenge wa uhuru jijini Dar es salaam yenye thamani ya zaidi ya shillingi
billion 7 .
Hayo yamesemwa na kiongozi wa mbio za mwenge capt. Ernest
Mwanossa wakati akikabidhi mwenge kwa kaimu mkuu wa wilaya ya kinondoni Bi:
Sofia Mjema mara baada ya kumaliza ziara ya mbio za mwenge katika wilaya ya
Ilala jijini Dar es salaam.
Mwenge huo uliwasili jijini Dar es salaam tarehe
25/06/2012 ukitokea mkoa wa kusini pemba na kuanza ziara ya mbio za mwenge siku
hiyo katika wilaya ya temeke, ilala na kukamilisha ziara hiyo leo katika wilaya ya Kinondoni.
Capt. Mwanossa amesema mwenge huo umebeba
ujumbe wa kuhamasisha watu kushiriki katika sensa ya watu na makazi , mchakato
wa katiba mpya na mapambano dhidi ya dawa za kulevya na ukimwi.
Nao wakuu wa wilaya za Temeke na Ilala wamesema Mwenge huo ni kwa ajili ya maendeleo ya mtu mmoja mmoja ikiwemo
kupambana na rushwa na kuchangia maendeleo katika sekta ya miundombinu na
elimu.
No comments:
Post a Comment