|
Eng.Charles Kitwanga-Naibu waziri ofisi ya makamu wa Rais |
|
Lila Mkila-Naibu Gavana-BOT |
|
Baadhi ya washiriki wa mkutano huo |
|
Baadhi ya washiriki wa mkutano huo |
|
Baadhi ya washiriki wa mkutano huo |
|
Baadhi ya washiriki wa mkutano huo |
|
Baadhi ya washiriki wa mkutano huo |
Serikali imeahidi
kuongeza kasi katika ulipaji wa deni lake kwa mfuko wa pensheni kwa watumishi
wa umma PSPF ili kufanikisha azma ya ulipaji wa mafao kwa wanachama wake kwa
muda muafaka
Mpaka sasa PSPF inaidai serikali shilingi bilioni 716
zinazotokana na mikopo ya serikali kwenye mfuko huo.
Naibu Waziri ofisi ya Makamu wa Rais Eng Charles Kitwanga akizungumza kwa niaba ya Makamu Wa Rais jijini Dar es
Salaam wakati wa ufunguzi wa mkutano
mkuu wa mwaka wa wadau wa mfuko huo amesema kuwa
serikali inatambua mchango wa mfuko huo katika kutekeleza azma ya kuwapatia
wananchi maisha bora hata baada ya kustaafu
Eng. Kitwanga amesema pia kuwa katika kuendeleza sekta ya hifadhi
za jamii serikali imeweka mikakati ya ulipaji wa madeni yake kwa mfuko huo
ikiwa ni pamoja na kuzihusisha sekta zisizo rasmi ili wananchi katika sekta
hiyo waweze kufaidika pia
Naibu gavana wa Benki kuu ya Tanzania bwana Lila Mkila
anataja anasema ucheleweshwaji wa fedha zilizowekezwa na mifuko hiyo
unachelewesha ulipaji wa pensheni kwa wastaafu ambao ni wanachama wa mifuko
hiyo.
PSPF imeweza kuongeza mtaji kutoka biliono 36.4 kwa mwaka
2002 kufikia bilioni 994.4 kwa mwaka 2011 ukiwa na zaidi ya wanachama zaidi ya
laki 3 nchi nzima
No comments:
Post a Comment