Saturday, June 30, 2012

Jiji la Dar sasa kusafishwa kwa teknologia mpya

Said Meck Sadick, Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam

Gari lenye mtambo maalum wa kuzolea taka





Jiji la Dar es Salaam limeanza mkakati wa kukusanya taka kwa kutumia mitambo maalum ya kuzoa taka na hata kuzisaga pamoja na kusafisha maeneo hayo ili kuboresha hali ya usafi katika jiji hilo. Jiji hilo limekuwa kati ya mikoa yote likiongoza kwa uchafuzi wa mazingira unaotokana na ongezeko la watu kwenye Jiji hilo.

Maeneo yanayoonekana kuwa machafu kwa wingi ni pamoja na vituo vya mabasi pamoja na maeneo ya masoko ambayo mara nyingi yanaonekana kushindwa kufanyiwa kazi kikamilifu hivyo kufanya jiji hilo kuendelea kuchafuka.

Mkuu wa mkoa wa dar es salaam Said Meck Sadick  amekiri kuwepo na uchafuzi huo lakini anasema kuwa ni jukumu la kila mwananchi kukusanya takataka katika sehemu zinazotakiwa pamoja na kuzilipia kama ambavyo sheria za serikali ya mitaa zinavyoagiza.

Kampuni tatu za kutoa huduma za usafi zimepewa tenda katika manispaa ya Ilala ili kuboresha hali ya usafi hasa katika maeneo ya vituo vya mabasi pamoja na  masokoni hasa soko kuu la samaki la kimataifa Kivukoni.

No comments:

Post a Comment