Tuesday, May 12, 2015

TAARIFA KWA UMMA

---------- Forwarded message ----------
From: "Dismas Lyassa" <globalsourcewatch@gmail.com>
Date: 12 May 2015 14:25
Subject: TAARIFA KWA UMMA
To: "audax mutiganzi" <audmg2000@yahoo.com>, "Juma Kengele" <kengelej@gmail.com>, "Maxence M. Melo" <macdemelo@gmail.com>, "Subi" <subi.nukta77@gmail.com>, "MR MATEMBELE" <amsalawi@yahoo.com>, "Chemi Kadete" <chemiche3@yahoo.com>, <tbcnewsroom1@gmail.com>, <davidrm@yahoo.com>, <fastnewstz@gmail.com>, "Adam Gille" <Adam.gille@gmail.com>, "adadi rajabu" <rajabuadadi@gmail.com>, "Deogratius Rweyunga" <drweyunga@gmail.com>, "kiishweko orton" <kiishorton2000@yahoo.com>, "Jestina George" <jestinageorge@gmail.com>, "shamim a.k.a Zeze" <shamyomy@yahoo.com>, "mange kimambi" <mangekimambi@hotmail.com>, <itvnewsroom@hotmail.com>, "Luke Joe" <djlukejoe@gmail.com>, "Mubelwa T Bandio" <mutwiba80@yahoo.com>, "alex kassuwi" <kassuwi@gmail.com>, "Abubakar Faraji" <abufaraji@googlemail.com>, "Radio" <balina@africaonline.co.tz>, "Furaha Eliab" <furahanews@gmail.com>, "Adam Mzee" <thamani80@gmail.com>
Cc:

 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Ndugu Wanahabari
Uchaguzi Mkuu wenye lengo la kuwapata Madiwani, Wabunge na Rais nchini unatarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu nchini.

Nimekuwa nikitembelea vijiji na kata mbalimbali za Wilaya ya Kilombero. Hivi karibuni nilitembelea kata zote za wilaya, nilizungumza na wananchi, wengi wao walinishauri kugombea Ubunge. Wananchi wanaamini kuwa kwa pamoja tutaweza kuendeleza vema gurudumu la maendeleo kwa kasi zaidi.

 

Wananifahamu kama mtoto wa masikini mwenzao niliyewahi kuzunguka mitaani kupiga picha ili kuendesha maisha, mtoto wa masikini niliyewahi kuwa na ofisi ya kusafisha viatu vya watu eneo la Ubungo Maziwa kwa mzee Mrisho ili niweze kupata nauli ya kwenda shule wakati huo nasoma Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE).

 

Maisha nayafahamu vizuri na nina uchungu nayo, natamani kushirikiana na wananchi ili kuepukana na maisha duni. Katika maisha yangu kutokula au wakati fulani kutembea kwa miguu kwenda chuo CBE na kurudi nyumbani Ubungo Maziwa (nilikuwa naishi kwa dada), lilikuwa ni jambo la kawaida, kwani maisha yalikuwa magumu mno.

 

Sauti ya wananchi wa Kilombero

Kilio cha wananchi pamoja na mambo mengine ni kwamba wanahitaji kiongozi kijana mwenye nguvu za kuongoza, kiongozi mwenye ujuzi wa namna ya kuongoza na kutawala, kiongozi ambaye atakuwa bega kwa bega na wananchi katika harakati za kuwaletea maendeleo wananchi. Kiongozi ambaye anajua namna ya kuongoza, siyo namna ya kuhonga au kuwalisha yamini wapiga kura, kwani wanachohitaji watu wa Kilombero ni maendeleo, siyo zaidi. Hawahitaji kiongozi ambaye ni maarufu kwa kutembelea magari ya kifahari, wanahitaji huduma za kijamii kama shule, hospitali na wao wenyewe kusaidiwa namna ya kubuni miradi ya maendeleo.

 

Elimu yangu ya juu ni Stashahada ya Uzamili katika Uongozi na Utawala (Postgraduate Diploma in Leadership and Governance), kutoka Chuo cha Utumishi wa Umma-Dar es Salaam niliyohitimu Aprili 22, 2014. Hata hivyo nje ya elimu nimekuwa nikishughulika na masuala ya kijamii kupitia kufanya mikutano ya ana kwa ana na jamii katika masuala ya ujasiriamali, uchumba/ndoa na kadhalika.

 

Mojawapo sababu za wananchi kuamini kwamba ninaweza kushirikiana nao kwa ufanisi ni rekodi ambazo wananchi wenyewe wanazo juu yangu, kwani nimekuwa nao karibu katika mambo mengi ya maendeleo ikiwamo kushirikiana nao moja kwa moja au vikundi vyao hasa  vya walemavu, kina mama, vijana na kadhalika kama mshauri wao katika suala zima la namna ya kuviendesha na kuwaunganisha na taasisi au watu wa kusaidiana nao.

 

Kwa hivi sasa maeneo kadhaa ya Kilombero yanasaidiwa na mashirika mbalimbali yakiwamo ya nje, baadhi yake ni kutokana na jitihada zangu….nje ya uandishi wa habari, pia nimekuwa nikimiliki kampuni ya kuwaunganisha watu na vyuo vya nje ya Global Source Watch (GSW), ambayo imekuwa ikinipa fursa ya kujuana na watu wengi wa nje.

Nachukua fursa hii kutangaza rasmi kwamba nitachukua fomu ya kugombea Ubunge kutokana na kukidhi vigezo vyote ya kugombea nafasi hii kama ilivyojieleza katika Katiba ya Tanzania ibara ya 67.-(1) ambayo pamoja na mambo mengine inasema  "Bila ya kuathiri masharti yaliyomo katika ibara hii, mtu yeyote atakuwa na sifa za kustahili kuchaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge endapo-

(a)    ni raia wa Jamhuri ya Muungano aliyetimiza umri wa miaka ishirini na moja, na ambaye anajua kusoma na kuandika katika Kiswahili au Kiingereza;

 

Mimi ni mzaliwa wa Kijiji cha Mofu, wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro, Juni 26, 1976. Nimewahi kufanya kazi katika vyombo mbalimbali vya habari ndani na nje ya nchi ikiwamo the Guardian Limited kama mwandishi wa kujitegemea, Uwazi kama Mhariri, Leo ni Leo kama Mhariri wa Makala, Mwananchi kama Mwandishi wa makala baadaye mhariri wa jarida la ndani ya biashara, the Media Project (Marekani) kama mchangiaji nk.

 

Kwa sasa ni Kiongozi wa Utafiti hapa nchini (National Lead Researcher) wa taasisi ya kimataifa iitwayo Global Integrity yenye makazi yake Marekani, pia ni Mhariri Mtendaji wa gazeti la Mwanahabari, lakini maamuzi haya ya kugombea ubunge ni yangu binafsi hayana uhusiano wala hayataingiliana na sehemu yoyote ninayofanyia kazi.

 

Nimewahi kutembea katika nchi mbalimbali kwa lengo la kwa kusoma na kutembea, baadhi yake ni Marekani, Kenya, Uganda, Dubai, Thailand, India.

 

OMBI KWA WASAMARIA WEMA

Napenda kuchukua fursa hii pia kuwaomba wasamaria wema kuangalia namna ya kusaidiana na wananchi wa Kilombero kwani wakati huu njia nyingi hazipitiki kwa sababu barabara zimejaa maji kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha. Magari yamekuwa hayapitiki katika maeneo mengi ya Kilombero kwa sasa.

 

Kwa mfano sehemu kubwa ya barabara ya kutoka  Ifakara kwenda Mofu haipitiki, kiasi kwamba wagonjwa wamekuwa hawawezi kubebwa kupelekwa Ifakara ambako ndiko pekee kuna hospitali ya Wilaya, St Francis. Wapo baadhi ya wagonjwa wamekuwa wakibebwa kwa kutumia baiskeli na hata pikipiki, jambo ambalo limekuwa gumu hasa kwa wajawazito.

 

Magari ya abiriia hasa Noah zilizokuwa zikifanya safari kutoka na kuingia Ifakara kutoka vijiji mbalimbali vya Wilaya ya Kilombero yamesitisha safari kutokana na barabara kujaa maji. Yapo magari machache hasa ya mizigo ambayo nayo yanafika baadhi ya vijijini kwa shida yakiwa yamebeba mizigo na abiria hivyo kuhatarisha usalama wa wananchi.

 

Mvua zimeathiri pia kilimo, kwani mashamba mengi yamefurika maji, huku kukiwa na njaa kwa baadhi ya wanavijiji. Hivyo nachukua fursa hii kuiomba Serikali kuchukua hatua za haraka kusaidia wananchi wakiwamo wa vijiji vya Mofu, Ihenga, Mlimba, Chisano, Chita,  Mkula, Sanje, Uchindile na Utengule

 

Imetolewa leo tarehe 12, Mei 2015,

na Dismas Lyassa                                 
(Mtangaza nia ya kugombea Ubunge Jimbo la Kilombero kwa tiketi ya CCM)
0754 49 8972/0712183282 

 

No comments:

Post a Comment