Wednesday, July 25, 2012

NMB YA KABIDHI ZAWADI KWA WASHINDI WA JENGA NA NMB


Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasiliano NMB, Imani Kajula (kuhoto) akikabidhi zawadi kwa mshindi wa promosheni ya Jenga Maisha na NMB, Richard Makala ambaye amejishindia tani ya saruji katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Washindi wa Jenga Maisha na NMB katika picha ya pamoja na  Imani Kajula (mwenye suti) Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasilano.wakabidhiwa zawadi zao kutoka kushoto ni Victoria Marisel, Ramadhan Mgunya, Rehema Mohamed, Rose Mandera na Richard Makala
 
Baadhi ya wateja wa benki ya NMB wameendelea kujipatia zawadi mbalimbali ikiwemo Tani moja ya mifuko ya Cement pamoja na Mabati kupitia bahati nasibu inayoendeshwa na benki hiyo ijulikanayo kama Jenga Maisha Bora.
 
Akiongea wakati wa kukabidhi zawadi hizo Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasiliano wa benki hiyo Imani Kajula amesema kuwa wameamua kuanzisha bahati nasibu hiyo ili kuwajengea wananchi tabia ya kujiwekea akiba.

Baadhi ya wateja walioibuka na ushindi huo wamewataka wananchi kuachana na tabia ya kuweka fedha katika majumba yao  na badala yake wapende kujiwekea akiba za fedha zao katika mabenki.

Jumla ya wateja watano wameibuka na ushindi huo akiwemo Richard makala, Edgar Mandera, Zariah Sarungi na Ramadhan Mgunya wakazi wa jiji la Dar es salaam.

No comments:

Post a Comment