Hawa Bayuni |
Wafanyakazi wa kampuni ya simu ya mkononi ya
Airtel leo wamejitolea kwa hiari kuchangia damu ili kusaidia kitengo cha damu
salama kinachohudumia wananchi wenye upungufu wa damu.
Mwezi june kila mwaka hujulikana kama mwezi wa
kujitolea damu ambapo watu mbalimbali wanahimizwa kuchangia damu kwa hiari yao
ili kuiwezesha benki ya damu kuwa na akiba ya kutosha ya damu.
Akizungumza kwa niaba ya wafanyakazi wa kampuni
hiyo Hawa Bayuni kutoka kitengo cha utawala amesema wao kama wafanyakazi
wameungana na watanzania wengine kuchangia damu kwa Benki ya Damu nchini ili
kuiwezesha kuwahudumia watanzania.
Kitengo hicho cha benki ya damu kilicho chini ya
ofisi ya wizara ya afya kinahitaji lita 200 za damu ili iweze kuhudumia
wagonjwa waohitaji huduma hiyo.
No comments:
Post a Comment