Monday, July 23, 2012

MAENEO YA USWAHILINI CHANGAMOTO KWA MPANGO WA KUBORESHA MAENDELEO YA MAKAZI



Waziri Tibaijuka akiongea na wakazi wa Manzese
Mpangilio mbovu wa makazi katika maeneo ya uswahili katika majiji mbalimbali huenda yakaigharimu serikali katika mpango wake wa kuboresha makazi unaoratibiwa na wizara ya ardhi nyumba na maendeleo ya makazi

Licha ya kuwepo hali hiyo Waziri wa ardhi Nyumba na Maendeleo ya makazi Profesa Anna Tibaijuka amewatoa hofu wananchi kuwa watafanikiwa kwa kufuata mpango wa kuboresha makazi huku wakitafuta namna ya kuboreha makazi hayo.

Profesa Tibaijuka amewasili katika kata ya Manzese Mvuleni na kutembelea nyumba kadhaa zilizoanza kuboreshwa katikati mwa kata hiyo yenye idadi kubwa ya makazi yasiyopangika

Akiwa hapo akatoa ufafanuzi endapo kuna mpango wowote wa kuyavunja makzi hayo ili kujenga ya kisasa zaidi na akatolea ufafanuzi suala hilo

Wakazi wa maeneo hayo pamoja na kusifu uamuzi wa Waziri kufika katika maeneo hayo, wana mapendekezo yao kwa serikali huku wengine wakiwa na hofu ya kutegemea mkopo katika ujenzi wa makazi yao.

Wizara ya Profesa Tibaijuka bado ina kazi kubwa ya kuhakikisha wananchi wananeemeka na mradi wa kuboresha nyumba TAFSUS unaofanywa kwa kushirikiana na Mabenki mbalimbali, na kuhusiana na mlolongo mrefu wa kupata mkopo huyu hapa ni Bw. Twaha Ally Dima miongoni mwa wakazi waliofaidika na mpango huo, huku Mkurugenzi wa Benki ya Azania naye akigusia suala hilo

Ziara ya Profes Tibaijuka katika maeneo hayo yenye makazi duni yatuma ujumbe kwa wananchi kukubali mabadiliko katika makazi chini ya mkakati ulionzishwa na Waziri huyo wa sasa katika nyumba na makazi wakati akiwa Katika umoja wa mataifa.

No comments:

Post a Comment