Irene Isack, Mkurugenzi SSRA |
Hilo limetokana na wanachama wengi
kutaka kujitoa katika mifuko hiyo na baadae wanapopata matatizo wanataka kurejea
tena kitu ambacho kinaweza kusababisha matatizo kwa mfano wafanyakazi wa
mgodini.
Akizungumza na waandishi wa habari
jijini dar es salaam mkurungezi wa SSRA Irene Isack amesema kwa mujibu
wa marekebisho hayo mwanachama atapata
mafao yake pale atakapofikisha miaka ya kustaafu kwa hiari miaka 55 na kwa
lazima miaka 60.
Nao baadhi ya wakurugenzi
wa mifuko ya jamii Crescentius
Magori wa NSSF na William Erio wa PPF wamesema kuwa mwanachama anaweza kupata
mkopo wa nyumba kupitia michango yao.
Kwa mujibu wa Bi. Irene mwanachama haruhusiwi kuhama mfuko hata kama
akiwa mapumziko na iwapo atarejea atatakiwa kurudi kwenye mfuko wake wa awali
na mwanacha mpya ndo anaruhusiwa kuchagua mfuko huku mamlaka ikiwa imeandaa
kanuni za mafao ili kuboresha maslahi yao
No comments:
Post a Comment