Bw. Faustin Sungura |
Bw. Faustin Sungura |
Aliyekuwa Mgombea
wa ubunge katika jimbo la uchaguzi la Moshi mjini mwaka 2010 kupitia NCCR
MAGEUZI-Faustin Sungura amelalamikia Ucheleweshwaji wa kesi unaofanywa na
Mahakama kuu kanda ya Moshi.
Kesi hiyo
ilifunguliwa na Bw. Sungura dhidi ya mwanasheria mkuu wa serikali pamoja na Mbunge wa Jimbo hilo
Philemon Ndesamburo.
Alipokutana na
waandishi wa habari katika makao makuu ya NCCR Mageuzi , Sungura amedai kuwa mazingira
ya kuendesha kesi yake yametawaliwa na rushwa huku akimtuhumu jaji Moses Mzuna
wa mahakama kuu kanda ya Moshi anayesimamia kesi hiyo kuhusika katika kukwamisha kesi yake
Madai ya
msingi ya kesi hiyo ni kupinga kiasi kikubwa cha dhamana kulingana na mwenendo
wa mahakama kuu inayoendesha kesi yake
Pamoja na
hayo Bw.Sungura amesisitiza kuwa ukiukwaji wa wazi wa sheria unaofanywa na jaji
na kulingana na hali hiyo amechukua
uamuzi wa kuachana na mahakama na kutumia njia za kiutawala
Baadhi ya
Ngazi hizo za kitawala ni pamoja na kuandikia barua kwa Rais wa Jamuhuri ya
muungano wa Tanzania,jaji mkuu,mkurugenzi mkuu wa usalama wa taifa ,mkurugenzi
mkuu wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa na nyinginezo ili haki iweze
kutendeka juu yake.
Dennis Mwasalanga
No comments:
Post a Comment