Thursday, July 12, 2012

CWT YALAANI TAARIFA ZA POTOFU KUHUSU MGOGORO WAKE NA SERIKALI


Chama Cha walimu Tanzania CWT kimelaani taarifa za upotoshwaji kuhusiana na mgogoro baina yao na serikali huku kikisisitiza kuwa hakitaanza mgomo hadi pale siku zilizoombwa kuongezwa na kamati ya usuluhishi kumalizika.

Gracian Mukoba  ni Rais wa CWT  amezungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam na kusema kuwa bado wamekuwa wakiona umuhimu wa walimu nchini hivyo serikali haina budi kusikiliza kilio chao.

Chama hicho awali kiliweka bayana nia yake ya kuanza mgomo endapo serikali isingetimiza madai yake ya msingi. CWT pia imekanusha taarifa za kuwepo mgomo eneo lolote la Tanzania huku ikisisitiza kuwa hadi sasa umma na walimu watambue kuwa hawaruhusiwi kugoma wala kushawishi kuwepo kwa mgomo miongoni mwa walimu nchini.

No comments:

Post a Comment