Wednesday, July 18, 2012

CCM KUWACHUKULIA HATUA ZA KISHERIA WANACHAMA WANAOLETA MISUGUANO NDANI YA CHAMA

CHAMA Cha Mapinduzi CCM kimesema kitawachukulia hatua kali za kisheria  baadhi ya wanachama wake wanaosababisha msuguano ndani ya chama hicho.

CCM imetoa kauli hiyo baada ya uwepo kwa Taarifa kuwa ziara zinazofanywa na chama hicho hazina baraka za kichama na kwamba hazitambuliki na Katibu Mkuu wa Chama hicho Wilson Mukama hali inayozua mkanganyiko kwa wanachama wake.

CCM imekuwa ikifanya ziara za kichama inayofahamika kama Ziara ya Ahadi ni Deni kwa kuambatana na watendaji wake kwenye mikoa mbalimbali ya Tanzania  ikiwa ni sehemu ya mipango mikakati ya kutafuta ufumbuzi wa kutatua changamoto zinazokwamisha suala zima la kimaendeleo.

Kufuatia ziara za chama hicho ndipo unaibuka mkanganyiko kwa baadhi ya wanachama wake kudai kuwa fedha za ziara hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Chama hicho kupitia kwa Katibu wake wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye jambo linalomsukuma Nape kutoa kauli hiyo.

Nnauye amesema kuwa ziara hiyo inafahamika kiutawala na kwamba inabaraka zote za kichama na kubainisha kuwa watu hao wanalengo la kukidhoofisha chama hicho.
CCM imekwisha fanya ziara kwenye mikoa ya Njombe, Iringa, Mbeya, Kagera, Rukwa, Katavi ambapo kesho inatajia kufanyika Mkoani Kigoma.

No comments:

Post a Comment