Mabalozi 9 kutoka nchi za Afrika wametoa msaada wa dola elfu 6 na mia tano(shilingi za kitanzania milioni 10) kwa mke wa baba wa Taifa mama Maria
Nyerere kwa ajili ya kusaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu waliopo
butiama mkoani mara. Msaada huo utasaidia malazi kwa watoto hao ambao Mama Maria
Nyerere aliwachukua na kuwapa hifadhi pamoja na kuwasomesha kutokana na
mazingira magumu waliyokuwa wakiishi.
Mabalozi
hao wametoa msaada huo jijini Dar Es Salaam wakati wa ziara waliyoifanya mkoani
humo.
No comments:
Post a Comment