Saturday, July 14, 2012

MSAMA PROMOTIONS YATOA BAISIKELI KWA WALEMAVU


Habib Juma akipokea msaada wa baisikeli

Alex Msama - Mkurugenzi Msama Promotions

William Dahani mmoja wa waliopokea msaada huo


Wafanyabiasha na watanzania kwa ujumla wametakiwa kuendelea kuwasaidia watu wenye ulemavu ili waweze kujikimu na kutambua kuwa  wana nafasi kubwa ya kuwasaidia watua hao katika masuala mbalimbali.

Wafanyabiashara hao wametakiwa kutenga muda wao na kuwafikiria zaidi watu wenye ulemavu kuwasaidia kwa hali na mali kwani baadhi yao wamekuwa wakikata tamaa kutokana na ugumu wa maisha uliopo.

Akizungumza wakati wa kutoa msaada wa baiskeli kwa baadhi ya watu wenye ulemavu mkurugenzi wa kampuni ya msama promotion Alex Msama amesema kuwa kuna umuhimu mkubwa katika kuwasaidia watu hao na ndiyo maana kampuni yake ikahamua kutoa msaada huo.

Nao Habibu Juma na William Dahani, waliopata msaada huo, wameitaka jamii kuguswa na watu hao na kuwasaidia katika masuala mbalimbali

Watu hao wenye ulemavu wamekuwa wakihitaji misaada ya aina mbambali ikiwemo fedha, elimu, na ushauri ili waweze kupata nafuu ya ugumu wa maisha unaowakabili baadhi yao.

No comments:

Post a Comment